Tuesday, March 10, 2015

AKUTWA AMEUAWA NA KUNYOFOLEWA SEHEMU ZA SIRI




MTU MMOJA MKAZI WA UTURO WILAYANI MBARALI ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA CHARLES SIJAONA @ MATEMLA (55) ALIKUTWA AMEUAWA NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA KWA KUKATWA KITU CHENYE NCHA KALI SEHEMU ZA KICHWANI NA SHINGONI. AIDHA MWILI WA MAREHEMU ULIKUTWA UKIWA UMENYOFOLEWA SEHEMU ZA SIRI NA WATU HAO.
MWILI WA MAREHEMU ULIKUTWA NJE YA NYUMBA ALIYOKUWA AKIISHI MNAMO TAREHE 08.03.2015 MAJIRA YA SAA 01:00 USIKU HUKO KATIKA KIJIJI CHA UTURO, KATA YA MAPOGOLO, TARAFA YA ILONGO, WILAYA YA MBARALI, MKOA WA MBEYA.
CHANZO CHA MAUAJI HAYO BADO HAKIJAFAHAMIKA, JUHUDI ZA KUWATAFUTA WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILO ZINAENDELEA.
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI NYIGESA R. WANKYO ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MAHALI WALIPO WATU WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAO. AIDHA MSAKO/UPELELEZI WA KUWABAINI WALIHUSIKA KATIKA TUKIO HILI UNAENDELEA.

Ushirikina kamwe hauwezi kuinua soka Bongo

Shabiki wa Yanga akishangilia kwa mtindo wa kuvaa hirizi na kushika njiwa, vitu ambavyo hutumika sana na waganga wa kienyeji. 


Posted  Jumatatu,Marchi9  2015  saa 12:7 PM
In Summary
Moja ya ndoto hizo ni kuhakikisha Tanzania inafuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) kwani tangu Taifa Stars ifuzu mwaka 1980 hadi sasa haijafuzu tena.



KAMA zilivyo nchi nyingine za Afrika, soka la Tanzania bado lipo chini, ni nchi ambayo inajikongoja kukamilisha ndoto zake.
Moja ya ndoto hizo ni kuhakikisha Tanzania inafuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) kwani tangu Taifa Stars ifuzu mwaka 1980 hadi sasa haijafuzu tena.
Kumekuwa na juhudi mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanyika ili kuikomboa Tanzania na kuhakikisha inafuzu kushiriki fainali hizo.
Ni hivi karibuni tu tumeshuhudia harakati za Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kushirikiana na klabu ya Barcelona kuanzisha chuo cha soka kwa vijana wa umri mdogo mjini Kigamboni.
Mbali na taasisi hiyo, watu binafsi nao wamekuwa mstari wa mbele katika kuanzisha shule za soka lengo likiwa ni hilo hilo la kutengeneza vipaji vya soka ambavyo vitakuwa na maana kwa taifa.
Hata hivyo katika hali ya kushangaza wakati baadhi ya watu wakiamini kuwekeza kwenye soka la vijana wadogo, wengine wanawekeza katika mbinu nyingine ambazo kimsingi zimepitwa na wakati.
Mbinu hizo ni kuwa na imani za ushirikina ambao wapo baadhi ya watu katika klabu wanaoamini bila kujihusisha na ushirikina hawataweza kupata matokeo mazuri katika timu zao.
Inasikitisha kuona kwamba wapo watu ambao hudiriki kutumia fedha nyingi kwa ajili ya mambo ya ushirikina na kutaka kutengewa bajeti maalum ya mambo hayo.
Hili kwetu bado tunaliona kuwa ni tatizo kubwa ambalo kama halitafanyiwa kazi basi mipango yote ya maendeleo ya soka itaendelea kukwama.
Ni tatizo kubwa hasa inapobainika kwamba klabu kubwa na kongwe za Simba na Yanga ndizo zinazoongoza katika mambo haya ya ushirikina.
Kabla ya mechi ya ya jana, Jumapili, klabu hizo zilihama jijini Dar es Salaam, Simba waliweka kambi Zanzibar wakati Yanga wao wakaweka kambi Bagamoyo.
Hatuna tatizo na uamuzi wa klabu hizi kutoka nje ya jiji la Dar es Salaam kutokana na umuhimu wa mechi yao lakini inasikitisha pale unaposikia kwamba sababu ya kwenda huko ni kurahisisha mambo ya ushirikina.

Wednesday, February 25, 2015

JESHI LA KUJENGA TAIFA TAARIFA KUHUSU VIJANA WALIOHITIMU MAFUNZO YA JKT KWA KUJITOLEA NA KUDAI KUAJIRIWA NA SERIKALI




Jeshi la Kujenga Taifa lilianzishwa Julai 10, 1963 na serikali kwa lengo la kuwaweka pamoja vijana wa nchi hii na kuwapa malezi kuhusu uzalendo na umoja ili kuondoa dalili za matabaka zilizoanza kujitokeza katika jamii baada ya uhuru.

                Baadhi ya sababu za kuanzishwa kwa JKT ni:
         Kubadili fikra za vijana wa nchi hii kutoka ile hali ya ukoloni kutegemea nchi nyingine kuleta maendeleo.

·           Kukusanya nguvu za vijana wote wa nchi hii na kuzielekeza kwa umoja wao kufanya kazi pamoja kwa manufaa ya taifa.

         Kuwafunza vijana kujenga mshikamano na umoja wa kitaifa, ili kulinda uhuru wa Taifa lao.

Jeshi la Kujenga Taifa linaunganisha vijana bila kujali itikadi zao, dini, elimu, jinsia na mali ili kuwalea kuwa wazalendo kwa taifa lao na kupenda kuitumikia nchi yao.

Pamoja na dhana ya kufunzwa uzalendo, pia stadi mbalimbali za kazi hufundishwa kwa vijana hao ili waweze kujiajiri, pindi wamalizapo mkataba yao ya kujitolea kwa miaka miwili.

Serikali ilirejesha mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa vijana wa kujitolea mwaka 2001, baada ya kusitishwa mwaka 1994.

Masharti ya Kujiunga na JKT kwa vijana wa Kujitolea
Kijana kabla ya kujiunga na JKT hutakiwa kuyajua masharti na kuzifahamu taratibu za kujiunga  na kuelewa kuwa JKT halitoi ajira.

Moja ya kipengele cha masharti ya kujiunga na JKT kinasema kuwa ‘Kwa kipindi chote nitakachokua ndani ya Jeshi la Kujenga Taifa nitakuwa nafanya mafunzo ya kijeshi na ya stadi za kazi na maisha, na baada ya mkataba nitarejea nyumbani. Hivyo sitalidai Jeshi la Kujenga Taifa ajira, wala kulitaka linitafutie ajira/kazi’.

Kipengele hiki kinaainisha masharti ya makubaliano kati ya Jeshi la Kujenga Taifa na kijana kabla ya kujiunga na kupatiwa mafunzo ya awali ya kijeshi.

Aidha, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na viongozi wengine mara kadhaa wamekuwa wakisisitiza kuwa, JKT halitoi ajira.

Lakini hivi karibuni wakati nchi inaelekea kwenye uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge mwaka huu, umezuka mtindo wa makundi ya vijana waliopitia JKT katika Operesheni mbalimbali kuomba kuandamana kwenda Ikulu kudai ajira.

Madai yanayopingana na dhana ya JKT na kauli ya Mhe. Rais kuwa Jeshi la Kujenga Taifa haliajiri, bali vijana hujiunga kwa hiari kwa kujitolea na baada ya mkataba wa miaka miwili wanatakiwa kurejea walikotoka.

Aidha, Mhe. Rais Kikwete, amewahi kutoa agizo kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, taasisi za Serikali na kuziomba zile zisizo za kiserikali kutoa ajira kwa vijana waliopata mafunzo ya JKT kulingana na sifa za kijana na nafasi zilizopo.

Takwimu zinaonesha kuwa tangu kurejeshwa kwa mafunzo ya JKT mwaka 2001 hadi mwaka jana, jumla ya vijana 104,594 wamejiunga na JKT wakiwemo wavulana 76,832 na wasichana 27,762.

Katika kipindi hicho, jumla ya operesheni 13 katika mafunzo ya JKT zimefanyika, Operesheni hizo ni pamoja na Operesheni Mkapa mwaka 2001, Miaka 40 ya JKT mwaka 2002, Utandawazi mwaka 2004 na Operesheni Jiajiri mwaka 2005.

Zingine ni pamoja na Kasi Mpya mwaka 2006, Maisha Bora mwaka 2007, Uadilifu mwaka 2008, Kilimo Kwanza mwaka 2009 na Operesheni Uzalendo mwaka (2010), Miaka 50 ya Uhuru (2011), Sensa mwaka 2012, Miaka 50 ya JKT (2013) na Miaka 50 ya Muungano (2014).

Vijana wa Kujitolea walioajiriwa
Tangu mwaka 2003 hadi 2014 jumla ya vijana 24,708 wameajiriwa katika vyombo  vya ulinzi na usalama ambapo vijana 21,977 wakiwemo wavulana 17,307 na wasichana 4,670 wameajiriwa na Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Jeshi la Polisi vijana 3,965 wavulana wakiwa 2,943 na wasichana 1,022, Magereza vijana 2,139 wavulana 2,044 na wasichana ni 95, Zimamoto vijana 100 wavulana wakiwa ni 78 na wasichana ni 22 na taasisi zingine vijana 592

Vijana 1,622 wameajiriwa katika taasisi mbalimbali kama TANAPA, GEITA GOLD MINE, BANDARI na AFRICAN GOLD MINE.

Ni vema vijana hao wakatambua kuwa tatizo la ajira sio kwao peke yao, ni tatizo la ulimwengu mzima Tanzania ikiwemo, wanashauriwa kutumia stadi za kazi kujiajiri wenyewe.

Aidha, vijana hao watambue kuwa walikula kiapo cha UTII, wakati wa kuhitimu mafunzo ya JKT, hivyo suala la kuandamana ni kinyume cha kiapo chao. Vijana hao walitumikia Jeshi la Kujenga Taifa Operesheni za nyuma na kumaliza mkataba wa miaka miwili. Shinikizo lao la kulazimisha ajira kwa kuandamana ni kinyume cha sheria za nchi.

Kwa maelezo ya hapo juu utaona kuwa Jeshi la Kujenga Taifa, halina dhamana ya kuajiri bali kufunza vijana wa taifa hili umoja, stadi za kazi na uzalendo baada ya hapo wenye sifa za kuajiriwa hupata ajira katika taasisi mbalimbali za serikari na binafsi.

Taarifa hii Imetolewa na Makao Makuu
ya Jeshi la Kujenga Taifa.



Wednesday, February 18, 2015

Yanga, Azam vitani ligi kuu Tanzania Bara


Vita ya kugombea usukani wa ligi kuu ya Tanzania Bara kati ya wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya vilabu ya Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kati za Azam FC na Yanga inaendelea Alhamis.
Baada ya kushinda mechi zao za CAF nyumbani,Yanga ikiwafunga BDF XI ya Botswana (2-0)
katika kombe la Shirikisho na Azam ikiwafunga El-Merreikh ya Sudan (2-0)
katika kombe la Klabu Bingwa Afrika, timu hizo sasa zinaelekea nguvu katika mechi za
ligi, ikiwa pia ni kama sehemu ya maandalizi ya mechi zao za marudiano za
ugenini.
Yanga watasafiri hadi Botswana na Azam wataenda Khartou, Sudan wakitafuta
ushindi ili kusonga mbele baada ya Juma moja lijalo. Kuelekea mechi zao za Ligi Kuu Alhamis, kila timu
ina pointi 25,Azam ikiongoza kwa tofauti ya goli moja. Yanga itacheza na Tanzania Prisons mjini
Mbeya na Azam watacheza na Ruvu Shooting mkoa wa Pwani.
Kocha wa Yanga, Hans Pluijm ametamba kushinda, huku akikabiliwa na kibarua kigumu kingine dhidi ya Mbeya
City wikiendi hii mkoani Mbeya, kwa lengo la kuongoza ligi yenye ushindani mkubwa.
Akizungumza jana, msemaji wa Azam, Jafar Iddi amesema baada ya kuwafunga Mtibwa
Sugar 5-2 majuma mawili yaliyopita, sasa ni Azam ya Ruvu Shooting katika jitihada za kukaa mbali na Yanga katika msimamo

Thursday, January 29, 2015

BINTI WA MIAKA 22 ASHINDA MILIONI 100 ZA PROMOSHENI YA JAYMILLIONS YA VODACOM

Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(katikati)akifafanua jambo kuhusiana na mshindi wa shilingi Milioni 100/-kupitia promosheni ya JayMillions inayoendeshwa na kampuni hiyo ambapo Mkazi wa kilolo mkoani Iringa Bi.Uwezo Magedenge aliibuka na ushindi wa kitita hicho katika droo ya 14 iliyochezeshwa jijini Dar es Salaam leo,Wengine ni Msimamizi wa Michezo ya Kubahatisha Tanzania Mrisho Millao(Kushoto) na Afisa wa kampuni hiyo Pristin Lyatonga.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay kwenda 15544.

Mkazi wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Uwezo Magendenye (22) , leo ameibuka mshindi wa kwanza wa shilingi milioni 100 katika droo ya kumi na nne ya promosheni ya Jaymilioni inayoendeshwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania.

Magedenge binti mwenye umri wa miaka 22 ambaye ni mhudumu wa mapokezi katika nyumba ya wageni ya Luganga Lodge iliyopo wilayani Kilolo amesema kuwa amepokea taarifa hizi kwa furaha akiwa kazini na amefurahia ushindi huu ambao anaamini utabadilisha maisha yake kwa kiasi kikubwa.

“Katika maisha yangu nimeishapitia mambo mengi nahangaika na maisha hadi kufikia hapa nilipo nikiwa mhudumu kwenye nyumba ya wageni.Kwa ushindi huu naamini nitafungua shughuli zangu za biashara ikiwemo kuanzisha biashara ya maduka ya M-Pesa pia kufungua nyumba yangu ya kulala wageni na kusaidia ndugu zangu ambao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za maisha”.Alisema.

“.Nashukuru Vodacom kwa kuleta promosheni hii ambayo naamini itabadilisha maisha yangu na namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniona na kusikiliza sala zangu .

Aliongeza kuwa kwa muda mrefu amekuwa akishiriki kwenye promosheni mbalimbali na hajawahi kufanikiwa kwa ushindi huu anaamini kuwa promosheni hizi hususani za Vodacom ni za kweli na amewataka wateja wote kushiriki ili kutopoteza bahati zao za kujishindia mamilioni ya fedha na kubadilisha maisha yao.

Akiongea muda mfupi baada ya kutangazwa mshindi, Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania,Rene Meza amempongeza mshindi na kuwahimiza wateja wote kuchangamkia promosheni hii kwa kuhakikisha wametuma neno JAY kwenda namba 15544 ili kutopoteza nafasi zao za kushinda pia alisema kuwa njia nyingine ya kushinda ni kutuma neno AUTO kwenda namba 15544 iwapo simu haina fedha ambapo mteja akiweka fedha anakatwa shilingi 300/-.

Naye Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania alisema kuwa tangu promosheni hii ianze mapema mwezi huu tayari wateja 2 wamekwishajishindia milioni 10 na wateja watano wameishajishindia shilingi milioni moja kila mmoja na maelfu wengine tayari wamejishindia muda wa maongezi.

“Promosheni hii itadumu kwa muda wa siku mia moja hivyo leo ni droo ya kumi na nne hivyo bado kuna mabilioni ya fedha yamewasubiri watanzania,wanachopaswa kufanya ni kuhakikisha kila siku wameangalia kama namba zao zimeibuka na ushindi kwenye droo ya siku kwa kutuma neno Jay kwenda namba 15544.

Thursday, January 29, 2015

BUSARA ZA MICHAEL WAKUDATA.

Friday, January 23, 2015

Ligi kuu Tanzania kuendelea Jumamosi



 
Ligi kuu ya Tanzania itaendelea Jumamosi hii huku mechi kadhaa zikichezwa ikiwemo ile kati ya bingwa mtetezi na wawakilishi wa nchi katika michuano ya klabu bingwa Afrika, Azam FC na Simba Sports Club ikiwa chini ya kocha Mserbia, Goran Kopunovic.
Azam inaongoza ligi ikiwa na pointi 20 na baada ya mechi yao na Simba itaenda Jamhuri ya Kongo (DRC) kwa ajili ya kucheza mechi za majaribio kwa ajili ya mechi yao na vigogo wa Sudan, El-Merreikh katika mechi ya kwanza klabu bingwa Afrika itakayochezwa Dar es Salaam kati kati ya mwezi ujao.
Mabingwa wa zamani wa Tanzania na wawakilishi wa nchi katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika, Yanga, ikiwa ya nne katika msimamo na alama (points) 15, watacheza na Polisi Morogoro wakati Mtibwa Sugar, ikiwa ya pili na alama 17, watacheza na Ruvu Shooting.
Mechi nyingine ni kama ifuatavyo
Stand United vs Coastal Union-Uwanja wa Kambarage,Shinyanga
Kagera Sugar vs Ndanda-Uwanja wa Kaitaba, Kagera
Mbeya City vs Tanzania Prisons-Uwanja wa Sokoine, Mbeya

Ishu ya Wema Sepetu kuhusu kumdai Diamond, majibu ya Wema ni haya hapa


sptUkubwa wa story hii ambayo jana aliizungumzia Martin Kadinda, Meneja wa Wema Sepetu imefanya millardayo.com kumtafuta Wema ili kuujua undani zaidi juu ya ishu hii ambayo ilichukua headlines kubwa Magazetini na mitandaoni pia.
Kwenye Exclusive Interview, Wema Sepetu amesema haya;
Taarifa hii imenishtua sana maana asubuhi ya jana nimekuta kwenye gazeti wameandika nikashangaa yaani hapa nimekaa kwa sababu muda mwingi siendeshi mimi akaunti yangu ya twitter, anaiendesha mtu wangu wa blog Bestizo maana nilikua nataka kutoa tamko-- Wema Sepetu.
Nilishasema ukurasa huu tulishaufunga na nilishasema haiwezi kujirudia tena, nashangaa watu wanarudi na maneno yale yale maana nimekaa kimya kwa kila kitu ili kuepuka haya maneno
Hakuna kitu ambacho namdai Diamond,hakuna siku hata moja nimefikiria kwenda kumshtaki Diamond labda kama kungekua kuna kitu chochote,yaani labda kungekua na ukweli wa kitu chochote siwezi kupoteza muda wangu kwenda polisi,sijawahi kufanya kitu cha namna hii hizi taarifa zimenishtua sana
Sijawahi kujiunga VICOBA maana sivijui, nilikua nimekaa na mtu akanambia labda Wema hujui  hawa watu wa VICOBA wanajaribu kujitangaza kwa njia hii na kutengeneza hii kitu kwamba VICOBA wanaweza kukopa hadi Milioni kumi… kwanza mimi siwezi kukopa Milioni 10“– Wema Sepetu.

Wednesday, January 21, 2015

Daladala ziligoma leo Arusha, ni Bodaboda tu barabarani…


BODAWaendesha bodaboda wa Arusha leo wamejikuta kwenye jukumu la daladala kusafirisha abiria baada ya mgomo wa daladala uliofanywa leo maeneo ya mji huo sababu ikitajwa ni kuanzishwa kwa route mpya wanayotakiwa kuanza hivi sasa kutoka Njiro na Moshono kuelekea mjini.
Wakazi wengi wa mji huo leo wamelazimika kutembea kwa miguu huku wengine wenye uwezo wakitumia usafiri wa bodaboda.
Bodaboda
Ripota wa Blog ya Michuzi ambaye ameripoti kuhusu story hii amesema yeye pia alikuwa mmoja ya walioathirika kutokana na mgomo huo

Sunday, January 18, 2015

HALMASHAURI YA JIJI LA MBEYA YATOA UFAFANUZI WA SINTOFAHAMU UKARABATI WA BARABARA YA IGANZO- KABWE.

Mhandisi wa Jiji la Mbeya, Laynas Sanya, akizungumza na vyombo vya habari Iganzo jijini Mbeya kuhusiana na ukarabati wa barabara ya Iganzo- Kabwe.

Mhandisi Msaidizi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Injinia Chaula, ambaye ndiye anayesimamia barabara hiyo akionesha namna Greda linavyopasa kusembua kifusi kabla ya kushindilia.

Afisa Mstaafu wa Idara ya ujenzi mkoani Mbeya,Betwel Mbelile akionesha kushangazwa na namna barabara hiyo inavyokarabatiwa.


Sehemu ya barabara ambayo imekamilika baada ya kumwagwa kifusi na kushindiliwa tayari kwa kuanza kutumika.


UONGOZI wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya umelazimika kutoa ufafanuzi wa sintofahamu kuhusu ukarabati wa barabara ya Iganzo- Kabwe kufuatia malalamiko ya baadhi ya wananchi.


Baadhi ya Wakazi wa Isanga walitoa malalamiko yako kwa vyombo vya habari wakilalamikia hatua zilizocghukuliwa na Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa kuamua kukarabatio Barabara ya Iganzo- Kabwe kwa kufukia vifusi vya mawe juu ya Lami huku wakihofia mvua zinazonyesha kuweza kuharibu.


Kutokana na malalamiko hayo na kuripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari baada ya uongozi wa Jiji kushindwa kujitokeza ili kuyatolea ufafanuzi ndipo Mhandisi wa Jiji la Mbeya, Laynas Sanya, akalazimika kufika eneo la mradi na kuzungumza na vyombo vya habari.


Mhandisi Sanya alisema ukarabati unaofanyika katika barabara hiyo ni kwa ajili ya kupitika katika kipindi kifupi wakati Uongozi wa Jiji ukijipanga kufanya ukarabati mkubwa hivyo kulazimika kuziba kwenye sehemu zilizokuwa zimechimbika sana huku sehemu nzuri zikirukwa.


Alisema baada ya kifusi kumwagwa Greda hupita na kuvuruga sehemu ya Lami ilichini ikichanganya na kifusi kisha kushindiliwa vizuri hali itakayosaidia njia hiyo kupitika kirahisi na kurahisisha masuala ya usafiri kwa wakazi wa Jiji la Mbeya.


Aliongeza kuwa mbali na Halmashauri ya Jiji la Mbeya kukosa fedha za kujenga upya barabara hiyo pia ikio kwenye mazungumzo ya kuifanya Barabara hiyo kupandishwa hadhi na kuwa ya Mkoa.


Akizungumzia kuhusu vifaa na Ukandarasi alisema kazi hiyo inafanywa na Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa kufuata kanuni za manunuzi ya umma isipokuwa Vifaa vilikosekana na kulazimu kukodi kwa Mkandarasi wa kampuni ya China Communications Contractor Company Ltd(CCCC) na kufanya jumla ya gharama zote kufikia shilingi Milioni 37.


Mwisho.


Saturday, January 17, 2015

USA kuamua kuhusu ndoa za jinsia moja


mahakama ya Marekani kufanya uamuzi wa jumla kuhusu ndoa za jinsia moja nchini humo
Mahakama kuu nchini Marekani inatarajiwa kutoa uamuzi wa nchi nzima iwapo wapenzi wa jinsia moja wana haki ya kufunga ndoa.
Mahakama hiyo itatathmini suala hilo kwenye majimbo ya Kentucky, Ohio, Michigan, na Tennessee kati ya majimbo mengine 14 ambayo yamepiga marufuku ndoa za jinsia moja.
Mahakama hiyo pia itaamua ikiwa majimbo yatatambua ndoa za jinsia moja kutoka sehemu nyengine nchini humo.
Kukubaliwa kwa ndoa za jinsia moja kumeshuhudiwa nchini Marekani miaka ya hivi karibuni suala ambalo linaungwa mkono pakubwa na chama cha Democratic huku likikigawanya chama cha Republican.

Thursday, January 15, 2015

Baada ya Diamond kumtema kimwana Wema Sepetu Bob Junior inasemekana ndio kajitwika kimwana huyo picha zipo hapa


 
LICHA ya Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ kuwahi kufikishwa kortini na Mbongo Fleva, Raheem Rummy Nanji ‘Bob Junior, wamebambwa ‘live’ wakioneshana mahaba niue, Amani lina tukio zima.

Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akiwa mapajani mwa Mbongo Fleva, Raheem Rummy Nanji ‘Bob Junior'.

TUJIUNGE TEGETA, DAR
Ishu hiyo iliyopigwa chabo na paparazi wetu hivi karibuni lilijiri ndani ya Ukumbi wa Club 71 uliyopo Tegeta jijini Dar es Salaam ambapo Wema siku hiyo alimtambulisha msanii wake mpya anayesimamiwa na kampuni yake ya Endless Fame anayeitwa Ally Luna.


WAKUTANA
Katika tukio hilo, Wema ndiye aliyeanza kufika ukumbini humo akifuatana na timu yake, akiwemo Petit Man (kama kawa).


Muda mfupi baadaye, Bob Junior naye alifika ambapo alipokutana na Wema walianza kupeana mahaba huku wakigandana kwa zaidi ya dakika kumi.


Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ akizidi kupozi kimahaba na ‘Bob Junior'.

Mbali na Bob Junior, Wema alialika wasanii kibao kwa ajili ya kumsapoti ambao hata wao walipigwa butwaa baada ya kushuhudia tukio hilo.

Wakiwa katika chumba cha VIP, Wema aliendelea kuwa ‘veri klozi’ na Bob Junior hivyo kusababisha minong’ono ya hapa na pale.


MAPOZI
Katika tukio hilo, kilichowashangaza mashuhuda zaidi ni kitendo cha Wema kukaa mapajani kwa Mbongo Fleva huyo bila kujalia macho ya watu.


Wema Sepetu na ‘Bob Junior' wakiteta jambo.

SALAMU KWA DIAMOND NA ZARI?
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walikwenda mbali zaidi na kuanza kuhisi tabia hiyo ya Wema na Bob Junior ni salamu kwa aliyekuwa mwandani wake na kumwagana Nasibu Abdul ‘Diamond’ na ‘bebi’ wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘Zari’.


“Hapa naona kama sielewielewi maana ni mara ya kwanza kumwona Wema na Bob Junior wakigandana kiasi hiki tangu walipopelekana mahakamani kipindi kile na ukizingatia Sharobaro (Bob Junior) alikuwa hasimu wa Diamond aliyekuwa mpenzi wa Wema kipindi hicho,” alisema mmoja wa mastaa wakubwa (jina linahifadhiwa). Akaongeza:

Wema Sepetu akimchumu ‘Bob Junior.

“Nakuhakikishia hizi ni salamu kwa Diamond na yule Zari wake. Hapa Wema anajua kabisa salamu zitawafikia.”

Baadhi ya mastaa hao walionekana kulaani tukio hilo na kujaribu kumtahadharisha Wema juu ya ukaribu huo kwani kama Diamond atagundua atajua ni ishu za kulipizana visasi.


“Kwa vyovyote Diamond akigundua jambo hili litamfanya ukaribu wake na Wema kuzidi kuwa mgumu na kuurejesha ni ndoto kama wana mpango wa kurudiana.”


WENYEWE WANASEMAJE?
Paparazi wetu alipojaribu kuwadodosa wawili hao juu ya uhusiano wao, kila mmoja aliishia kucheka tu bila kutoa majibu ya kueleweka.


DAKTARI AMUONYA WEMA
Wakati huohuo, mmoja wa madaktari wa mastaa Bongo (jina lipo) amemuonya Wema kuhusu masuala ya mapenzi kwamba, kama ni kweli ameanzisha uhusiano mwingine si vizuri kwani bado akili yake haijatulia tangu amwagane na Diamond hivyo anahitaji muda ili kutuliza akili.


“Wema hatakiwi kuanzisha uhusiano wa kimapenzi kwa haraka, wala si vizuri kulipiza kisasi kwani anaweza kujikuta pabaya zaidi, haya mambo ya mapenzi yanatesa sana mastaa wengi na nimekuwa nikiwapa huduma za kisaikolojia,” alisema dokta huyo kwa sharti la kutotajwa gazetini.

TUJIKUMBUSHE
Mwaka 2011, Mahakama ya Mwanzo Kinondoni jijini Dar ilimhukumu Wema kwenda jela miezi sita au faini ya shilingi elfu 40 baada ya kupatikana na hatia ya kumtukana matusi ya nguoni Bob Junior ambapo alilipa faini na kuachiwa huru jambo lililoibua uhasama mkubwa kati yao.


Hivyo, tukio la kuonekana pamoja na kugandana kimahaba ni ishara njema kuwa sasa wapo vizuri na ule uhasama haupo tena!!

Saturday, January 10, 2015

WADAU WAOMBWA KUJITOKEZA UBORESHAJI HOSPITALI YA MKOA WA MBEYA.


Mganga mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, Dk. Glori Mbwile, akimkaribisha Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya pamoja na wageni waliowatembelea. 
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dk. Seif Mhina akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya pamoja na wageni wao kutoka Benki ya NMB Mbeya.
Afisa Uhusiano wa Serikali wa Benki ya NMB Kanda ya Mbeya, Focus Lubende, akifafanua baadhi ya mambo kwa watumishi wa hospitali ya mkoa wa Mbeya.
Meneja wa NMB Kanda ya Mbeya, Lecresia Makiriye, akizungumza na Watumishi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya kuhusu lengo lao la kutembelea Hospitali hiyo.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dk. Seif Mhina akipokea msaada wa magodoro kutoka kwa meneja wa NMB Kanda ya Mbeya.
 Mganga mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, Dk. Mbwile akipokea msaada wa magodoro kutoka kwa Meneja wa NMB kanda ya Mbeya.
Baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya wakisaidiana na uongozi wa hospitali kupokea msaada wa magodoro kutoka kwa wafanyakazi wa NMB.
Baadhi ya Wauguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya wakifuatilia kwa makini zoezi la makabidhiano wa magodoro.

WADAU wa Maendeleo mkoani Mbeya wametakiwa kujitokeza katika kuchangia uboreshaji wa Hospitali ya Mkoa ikiwa ni pamoja na ununuzi wa vifaa na vitanda katika Wodi mpya ya watoto.
Aidha imeelezwa kuwa wadau wa sekta binafsi kushiriki katika shughuli za maendeleo ni utekelezaji wa adhma ya Serikali ya uanzishwaji wa mfumo shirikishi baina ya serikali na sekta binafsi(PPP).
Wito huo ulitolewa hivi karibuni na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dk. Seif Mhina, alipokuwa akipokea msaada wa magodoro kwa ajili ya kulalia wagonjwa kutoka Benki ya NMB Kanda ya Mbeya.
Dk. Mhina alisema wadau zaidi wanatakiwa kujitokeza kuchangia ukarabati na maboresho ya Hospitali ya Mkoa wa Mbeya ili iweze kutoa huduma kwa wananchi kwa kiwango sahihi na kwa wakati muafaka baada ya miundombinu muhimu kukamilika.
Alisema kutokana na msaada wa magodoro 17 uliotolewa na wafanyakazi wa Benki ya Nmb, hivyo uongozi wa Hospitali unapaswa kutoa kipaumbele cha matibabu  kwa watumishi wa benki hiyo kwa kuwekewa mfumo maalumu utakaowawezesha kutopanga foleni kusubiri matibabu.
“Labda ni waagize watumishi wenzagu kuanzia leo watumishi wa Nmb wakifika Hospitalini hapa kwa lengo la kutibiwa wapewe kipaumbele ikiwezekana wakaingizwa kwenye mfumo wanaotibiwa wagonjwa wa bima ya afya” alisema Dk. Mhina.
Kwa upande wake Mganga mkuu wa Hospitali hiyo, Dk. Glori Mbwile, akitoa shukrani kwa msaada wa magodoro alisema bado kunachangamoto ya ujenzi wa njia za kupitishia wagonjwa pamoja na kununulia vifaa katika Wodi ya watoto.
Alisema wodi mpya ya watoto inahitajika kuwa na vitanda 80,magodoro na vifaa vingine vinavyopaswa kuwemo wodini vyenye thamani ya shilingi Milioni 160 hivyo msaada zaidi wa wadau unahitajika ili kukabiliana na changamoto hiyo.
Awali akizungumza kabla ya kukabidhi msaada wa magodoro, Meneja wa Kanda wa Benki ya NMB, Lecrisia Makiriye, alisema mara nyingi benki huangalia maeneo ambayo wateja wake wanapatikana kama katika sekta za elimu na afya ili kusaidia kupunguza changamoto zinazokuwepo.
Alisema Wafanyakazi wa Benki waliamua kuchangishana na kununua magodoro 17 pamoja na fedha taslimu shilingi Milioni 2 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa njia za kupitishia wagonjwa.
“Tunawiwa kuona taasisi zinazohudumia umma tunazichangia ili kupunguza changamoto kwa kuisadia Serikali ndiyo maana tukanunua magodoro haya machache ingawa tunaona bado hayajamaliza tatizo pamoja na fedha za kujengea njia za kupitishia wagonjwa” alisema Meneja huyo.
Mwisho.

Monday, January 5, 2015

Sikiliza U Heard inayohusu uhusiano wa AY na Sitti Mtemvu

Sikiliza U Hear inayomuhusu mzee wa Comesho Ambwene Yesaya a.k.a AY na aliekuwa na kujivua taji la Miss Tanzania 2014 Sitti Mtemvu 


Mwalimu: Profesa Muhongo ajitathmini kwanza badala ya kuendelea na ziara


Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ametakiwa kujitathimini kwanza katika utendaji wake wa kazi kuliko kuwaongezea hasira Watanzania kutokana na kutumia pesa za umma kufanya ziara wakati anakabiliwa na kashfa ya fedha kuchotwa kwenye akaunti ya Tegeta Escrow.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara jijini Mwanza juzi, naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Zanzibar, Salum Mwalimu, alisema ni wakati wa Profesa Muhongo kuacha kuzunguka mikoani akitumia pesa za umma wakati anafahamu alichofanya kwenye Escrow.

“Kwanza tunashangazwa na Rais Jakaya Kikwete, kushindwa kumtolea maamuzi magumu Profesa Muhongo, amemchukulia hatua Profesa Anna Tibaijuka na kumuacha waziri huyu ambaye anatumia pesa za umma kuzungukia mikoani akidai atawapa Watanzania umeme ,” alisema Mwalimu.

Aidha akizungumzia uboreshaji wa daftari la wapigakura kwa kutumia mfumo wa kielektroniki wa Biometric Voters Registration (BVR), alisema haitakiwi wanajeshi wasimamie zoezi hilo.

Mwalimu alisema kutumia wanajeshi kusimamia uandikishaji na uchaguzi mkuu mwaka huu, ni kuwatisha wananchi ambao wanahitaji kufanya uchaguzi kwa amani bila vitisho vya wanajeshi.

Akiwa wilayani Ukerewe katika kisiwa cha Ukara, Mwalimu aliwapongeza wananchi wa kisiwa hicho kwa kuipa Chadema ushindi wa vijiji saba kati ya nane ikilinganishwa na hapo awali ilikuwa na uongozi katika vijiji viwili kabla ya uchaguzi mwezi uliopita.

Alisema Watanzania hawatakiwi kurudi nyuma badala yake waongeze umoja na mshikamano walioonyesha katika uchaguzi wa serikali za vijiji na mitaa ili kuing'oa CCM madarakani, huku mwenyekiti wa Chadema wilayani humo, Jacob Munyaga pamoja na mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemli, wakieleza mikakati ya chama hicho kupata ushindi wa kishindo.