Tuesday, March 10, 2015

Ushirikina kamwe hauwezi kuinua soka Bongo

Shabiki wa Yanga akishangilia kwa mtindo wa kuvaa hirizi na kushika njiwa, vitu ambavyo hutumika sana na waganga wa kienyeji. 


Posted  Jumatatu,Marchi9  2015  saa 12:7 PM
In Summary
Moja ya ndoto hizo ni kuhakikisha Tanzania inafuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) kwani tangu Taifa Stars ifuzu mwaka 1980 hadi sasa haijafuzu tena.



KAMA zilivyo nchi nyingine za Afrika, soka la Tanzania bado lipo chini, ni nchi ambayo inajikongoja kukamilisha ndoto zake.
Moja ya ndoto hizo ni kuhakikisha Tanzania inafuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) kwani tangu Taifa Stars ifuzu mwaka 1980 hadi sasa haijafuzu tena.
Kumekuwa na juhudi mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanyika ili kuikomboa Tanzania na kuhakikisha inafuzu kushiriki fainali hizo.
Ni hivi karibuni tu tumeshuhudia harakati za Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa kushirikiana na klabu ya Barcelona kuanzisha chuo cha soka kwa vijana wa umri mdogo mjini Kigamboni.
Mbali na taasisi hiyo, watu binafsi nao wamekuwa mstari wa mbele katika kuanzisha shule za soka lengo likiwa ni hilo hilo la kutengeneza vipaji vya soka ambavyo vitakuwa na maana kwa taifa.
Hata hivyo katika hali ya kushangaza wakati baadhi ya watu wakiamini kuwekeza kwenye soka la vijana wadogo, wengine wanawekeza katika mbinu nyingine ambazo kimsingi zimepitwa na wakati.
Mbinu hizo ni kuwa na imani za ushirikina ambao wapo baadhi ya watu katika klabu wanaoamini bila kujihusisha na ushirikina hawataweza kupata matokeo mazuri katika timu zao.
Inasikitisha kuona kwamba wapo watu ambao hudiriki kutumia fedha nyingi kwa ajili ya mambo ya ushirikina na kutaka kutengewa bajeti maalum ya mambo hayo.
Hili kwetu bado tunaliona kuwa ni tatizo kubwa ambalo kama halitafanyiwa kazi basi mipango yote ya maendeleo ya soka itaendelea kukwama.
Ni tatizo kubwa hasa inapobainika kwamba klabu kubwa na kongwe za Simba na Yanga ndizo zinazoongoza katika mambo haya ya ushirikina.
Kabla ya mechi ya ya jana, Jumapili, klabu hizo zilihama jijini Dar es Salaam, Simba waliweka kambi Zanzibar wakati Yanga wao wakaweka kambi Bagamoyo.
Hatuna tatizo na uamuzi wa klabu hizi kutoka nje ya jiji la Dar es Salaam kutokana na umuhimu wa mechi yao lakini inasikitisha pale unaposikia kwamba sababu ya kwenda huko ni kurahisisha mambo ya ushirikina.

No comments:

Post a Comment